Uchambuzi Linganishi Wa Maudhui Na Majukumu Ya Nyimbo Za Harusi Za Wadigo Na Waswahili
Abstract
Utafiti huu unahusu uchambuzi linganishi wa maudhui
na majukumu ya nyimbo za harusi za
Wadigo na Waswahili. Kazi hii imegawanywa katika su
ra nne. Katika sura ya kwanza
tumeangazia maswala muhimu ya utafiti wetu. Tumeele
zea swala la utafiti, madhumuni na
nadharia tete zilizotuongoza. Aidha, sababu za utaf
iti zimeelezwa pamoja na upeo na mipaka.
Msingi wa nadharia wa utafiti umefafanuliwa na yali
yoandikwa kuhusu mada yalijadiliwa.
Mwisho, mbinu za utafiti zimebainishwa na uchanganu
zi wa data umefanywa. Katika sura ya
pili, tumeshughulikia utaratibu wa ndoa na harusi z
a Wadigo na Waswahili. Aidha, katika sura
ya tatu tumeangazia maudhui na majukumu katika nyim
bo za harusi za Wadigo na Waswahili.
Mbali na haya, pia tumeshughulikia walengwa wa ujum
be katika nyimbo hizi. Mbali na hayo,
tumelinganisha na kutofautisha maudhui na majukumu
yanayojitokeza katika nyimbo za harusi
za Wadigo na Waswahili. Sura ya nne, ambayo ndio ya
mwisho, tumejikita katika matokeo ya
utafiti, changamoto tulizokumbana nazo na pia tumet
oa mapendekezo ya utafiti wa baadaye
kuhusu mada hii
Publisher
University of Nairobi