• Login
    • Login
    Advanced Search
    View Item 
    •   UoN Digital Repository Home
    • Theses and Dissertations
    • Faculty of Arts & Social Sciences, Law, Business Mgt (FoA&SS / FoL / FBM)
    • View Item
    •   UoN Digital Repository Home
    • Theses and Dissertations
    • Faculty of Arts & Social Sciences, Law, Business Mgt (FoA&SS / FoL / FBM)
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Mtindo unavyoendeleza maudhui katika natala

    Thumbnail
    View/Open
    Abstract (10.09Kb)
    Full text.pdf (399.0Kb)
    Date
    2013-11
    Author
    Kanyua, Murungi G
    Type
    Thesis
    Language
    other
    Metadata
    Show full item record

    Abstract
    Utafiti huu unahusu jinsi mtindo unavyoendeleza maudhui katika Natala (1997) ya Kithaka Wa Mberia. Tumeshughulikia vipengele vya kimtindo vya wahusika, matumizi ya lugha na maudhui katika ujenzi na uendelezaji wa ukombozi wa wanawake katika jamii iliyotawaliwa na mfumo wa ki-ubabedume unaojitokeza katika Natala. Tumetumia nadharia ya Ufeministi wa Kiafrika kuchanganulia masuala ya mwanamke, na nadharia ya umuundo kuchunguza vipengele vya kimtindo. Kazi yetu imegawanywa katika sura tano. Katika sura ya kwanza tumejadili somo la utafiti, madhumuni ya utafiti, sababu za kuchagua mada, upeo na mipaka, nadharia tete, misingi ya nadharia, yaliyoandikwa kuhusu mada na mbinu za utafiti. Katika sura ya pili tumeshughulikia historia fupi ya tamthilia, awamu za maendeleo ya tamthiliakipindi cha kabla ya ukoloni, kipindi cha ukoloni na baada ya ukoloni. Aidha tumeshughulikia muhtasari wa Natala. Katika sura ya tatu tumechunguza mchango wa wahusika katika ujenzi na uendelezaji wa maudhui. Tumeangazia dhana ya wahusika, wahusika wakuu na wahusika wadogo, ulinganuzi wa wahusika, umakundi wa wahusika na dhima yao katika ujenzi wa maudhui. Sura ya nne imeshughulikia matumizi ya tamathali za usemi na kunga za fasihi na athari zake katika kuendeleza maudhui. Aidha tumechunguza mandhari yalivyohusishwa na matukio katika ujenzi na uendelezaji wa maudhui. Sura ya tano ni hitimisho la utafiti wetu. Tumejadili muhtasari wa matokeo na mapendekezo ya utafiti wa baaadaye.
    URI
    http://erepository.uonbi.ac.ke:8080/xmlui/handle/123456789/59975
    Citation
    Shahada Ya Uzamili Katika Chuo Kikuu Cha Nairobi, 013
    Publisher
    University of Nairobi
     
    linguistic and languages
     
    Collections
    • Faculty of Arts & Social Sciences, Law, Business Mgt (FoA&SS / FoL / FBM) [24364]

    Copyright © 2022 
    University of Nairobi Library
    Contact Us | Send Feedback

     

     

    Useful Links
    UON HomeLibrary HomeKLISC

    Browse

    All of UoN Digital RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Copyright © 2022 
    University of Nairobi Library
    Contact Us | Send Feedback