`Matatizo Ya Ukalimani:uchambuzi Wa Mahubiri Ya Kidini`

View/ Open
Date
1998Author
Ogonda, Joshphine O
Type
ThesisLanguage
enMetadata
Show full item recordAbstract
Tasnifu hii inashughulikia matatizo ya ukalimani ambapo kwa kuchambua mahubiri ya kidini, tumeweza kuyabainisha baadhi ya inatatizo hayo. Kazi yenyewe imegawanywa katika sura tano.
Sura ya kwanza ni utangulizi. Katika utangulizi wa sura hii tumeweza kutoa maelezo mafupi kuhusu historia ya ukalimani. Tumezungumzia pia kuhusu somo la utafiti, madhumuni ya tasnifu na haipothesia zilizotuongoza katika utafiti wetu. Zaidi ya hayo tumeweza kuangalia yaliyoandikwa kuhusu somo hili ambapo tuliweza kupitia kazi zilizoandikwa kuhusu tafsiri na ukalimani. Vilevile tumeweza kutoa sababu zetu za kuchagua somo hili, msingi wa kinadharia na upeo wa tasnifu. Hatimaye tumeweza kueleza njia tulizotumia katika utafiti wetu.
Sura ya pili inazungumzia masiala mbalimbali kuhusiana na ukalimani. Katika sura hii tumeweza kuangalia dhana ya ukalimani na kuilinganisha na tafsiri. Kwa kufanya hivyo tumeweza kuona tofauti na ushabihiano ulioko kati ya dhana hizi mbili. Mwisho tumeangalia aina mbalimbali za ukalimani.
Sura ya tatu inahusu uchambuzi halisi wa data tuliyokusanya. Katika sura hii tumezingatia matatizo ya kiisimu katika viwango vinne: fonolojia, sintaksia, leksia
na maana. Tuinetoa mifano kuonyesha vile makosa yanavysjitokeza katika kila kiwango.
Sura ya nne inashughulikia matatizo yasiyo ya kiisimu.
(iv)
Hapa turaejaribu kuoanisha matatizo haya na yale ya kiisumu ili kuona vile matatizo yasiyo ya kiisimu yanavyoweza kuchangia
yale ya kiisimu.
Sura ya tano ni hitimisho. Katika sura hii tumetoa maelezo ya kijumla kuhusu utafiti wetu na matokeo yake. Pamoja na hayo, tumetoa mapendekezo.
Citation
Master of Arts in Kiswahili,Publisher
University of Nairobi,
