• Login
    • Login
    Advanced Search
    View Item 
    •   UoN Digital Repository Home
    • Books
    • Faculty of Arts & Social Sciences (FoA&SS / FoL / FBM)
    • View Item
    •   UoN Digital Repository Home
    • Books
    • Faculty of Arts & Social Sciences (FoA&SS / FoL / FBM)
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Uwezeshaji lugha ili kuleta maendeleo: sera, utendaji na nafasi ya Kiswahili

    Thumbnail
    View/Open
    Abstract (7.613Kb)
    Date
    2014
    Author
    Michira, N,
    Iribe, Mwangi pI
    Mbatia, M
    Mutiga, J
    Type
    en
    Language
    en
    Metadata
    Show full item record

    Abstract
    Nafasi ya lugha za waliokuwa wakoloni Afrika kama vile; Kiingereza, Kifaransa na Kireno, imezisukuma lugha za Kiafrika hadi ukingoni katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi barani Afrika. Lugha za Kiafrika zimevurugwa na kutengwa katika msitari wa mbele wa uchumi wa nchi ambapo lugha hizi zinazungumzwa, jambo ambalo linaonekana kuwa mojawapo ya visababishi vya Afrika kutokuwa na maendeleo. Jambo hili limesasababishwa na nafasi ya lugha zilizokuwa zinatumiwa na wakoloni, kama vile Kiingereza, Kifaransa na Kireno na kuendelezwa na mtazamo wa waafrika wenyewe ambao huzidunisha lugha zao na kuamini kwamba wataweza kujiendeleza kupitia kumilisi vyema na kutumia lugha zilizotumiwa na serikali za kikoloni; jambo hili pamoja na wazo kuwa lugha ndiyo msingi au nguzo ya mchakato wa maendeleo ya namna yoyote ile. Swali la kujiuliza ni: Je, bara la Afrika linaweza kujipatia maendeleo yaliyo thabiti wakati wazungumzaji wanaendelea kutumia lugha ambazo zinaonekana kuzuia kuelimishwa pamoja na mawasiliano miongoni mwa watu wengi? Hivyo basi, lengo la makala haya ni kuangazia vile lugha inaweza kuwezeshwa ili kusaidia watumizi wake kushiriki katika shughuli za maendeleo ya nchi yao. Aidha inaendelea kuangazia njia ambazo zinaweza kutumiwa kuwezesha lugha ya Kiswahili nchini Kenya na katika eneo la Afrika Mashariki ili kuendeleza eneo hili wakati huu ambapo kuna katiba mpya na uundaji sera mpya nchini Kenya.
    URI
    http://hdl.handle.net/11295/80146
    Citation
    Michira N, IRIBEMWANGI PI, Mbatia M, Mutiga J. "Uwezeshaji Lugha ili Kuleta Maendeleo: Sera, Utendaji na Nafasi ya Kiswahiili.". In: Ukuzaji wa Kiswahili. Nairobi: Focus Publishers Limited; 2014.
    Publisher
    University of Nairobi
    Collections
    • Faculty of Arts & Social Sciences (FoA&SS / FoL / FBM) [1299]

    Copyright © 2022 
    University of Nairobi Library
    Contact Us | Send Feedback

     

     

    Useful Links
    UON HomeLibrary HomeKLISC

    Browse

    All of UoN Digital RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    Copyright © 2022 
    University of Nairobi Library
    Contact Us | Send Feedback